Ziara ya Rainer Zietlof imeanzia kwenye mji uliopo North Cape nchini Norway inategemewa kumalizika Cape Agulhas nchini Afrika Kusini,timu hii itaweka rekodi ya tatu ya dunia pamoja na wenzake Matthias Prillwitz na Marius Biela.
Ziara hiyo waliianza Sept 21 ambapo wakifika Afrika kusini watakuwa wametembea nchi mbalimbali kama Norway,Finland,Sweden,Denmark,Ujerumani,Jamhuri ya Czech,Slovakia,Hungary,Serbia,Bulgaria,Turkey,Misri,Sudan,Ethiopia,Kenya na sasa Tanzania.
Rekodi nyingine aliyovunja ilikua ni ile ya Russtralia ambayo ilikua kutoka Malbourne hadi St.Petersburg kwa siku 17 na masaa 11,Mradi huu wa uendeshaji wa magari upo chini kampuni ya magari ya Tehama na Volkswagen ya Ujerumani,Slovakia na Afrika Kusini.
Facebook Blogger Plugin by Michapo Blog
Post a Comment