Baba mtarajiwa amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya kuishi bila kuwa na uso na kwa namna gani anahofia juu ya hali atakayozaliwa mtoto wake mtarajiwa.

Anaitwa Mohammad Latif Khatana, 32, kutoka Kashmir, India, hawezi kuona wala kufanya kazi kutokana na ngozi zilizofunika uso wake. Watu humkimbia barabarani kutokana na hali yake huku wakionekana kuogopeshwa nayo.


Kwa sasa ni mwenye faraja kutokana na ukweli kwamba mke wake ni mjamzito wa miezi saba, ila ana hofu labda huenda mtoto wake anaweza kuzailiwa akiwa anfanana naye.
Alisema: “Naingoja kwa hamu hii hali ya kuwa baba na kupata furaha ya maisha. Ila nahofu kila siku na kusali ili mwanangu asije kuzaliwa kama mimi.”
Latif, ambaye anaishi milimani na mke wake mwenye miaka 25 aitwaye Salima, eneo la Tuli Bana, ndani ya Jammu and Kashmir, huwa anatembea mpaka Srinagar mara nne kwa mwaka kwa ajili ya kuomba misaada na ili kupata hela.
Alizaliwa na kinundu kidogo kwenye uso wake ila kimeendelea kukua na ktengeneza tabaka kubwa la ngozi kwenye paji la uso wake, linalomfanya ashindwe kuona.
Anasema: “Mama yangu bado analia kila aniangaliapo, anajiona kama mtu mwenye kosa na anashindwa kuelewa kwa nini mtoto wake wa mwisho amekuwa hivi.”
Latif ni mdogo kati ya wakaka wawili na dada watatu huku yeye pekee akiwa na tatizo hilo.
Bila ndugu zake angeweza kuishi maisha ya upweke sana udogoni kutokana na kutokuwa na marafiki.
“Hakuna aliyetaka kucheza na mimi utotoni,” akaongeza. “Wavulana kijijini kwangu walikuwa wananipiga na kunitesa kila siku. Nilipoteza jicho langu la kushoto nilipokuwa na miaka minane na wakawa wananiita mjinga mwenye jicho moja.”
Alipokuwa kijana Latif alikumbana na changamoto mbalimbali za kimaisha. Ni mtu mwenye nguvu zake ila kutokana na kushindwa kuwa anaona na kwa namna uso wake ulivyo hakuna aliyeweza kumpa kazi.
Alisema: “Ningependa kufanya kazi ya uhakika kama wanaume wengine wanavyofanya ili kuweza kuzitunza familia zao, ingenifanya nijisikie fahari sana, ila hakuna aliyenipa nafasi. Inabidi niombe  na naamini watu wanaweza nisaidia ili niweze kulisha familia yangu.”
Miaka minne iliyopita Latif alikutana na mwanamke wa maisha yake, awali wazazi wake walijitahidi sana kumtafutia mke ila hakuna msichana liyejitokeza, mpaka Latif aliposikia kuhusu Salima.

“Mke wangu ana mguu mmoja tu na kwa muda mrefu amekuwa akitafuta mume, punde tulipokutana tulijua tulikuwa sahihi kwa kila mmoja wetu,” anakumbuka. “Wote tulikuwa hatujakamilika, hakika tuliendana.”
Walioana kwenye harusi ya Kiislamu wakiwa na wageni 400 mnamo August 2008 na wamekuwa wenye furaha toka kipindi hicho.
Akaongeza: “Najiona nimebarikiwa sana kwa kukutana na Salima, ni mwanamke mzuri kwangu.
“Sasa naona kawaida nina mke, ni kitu kikamilifu zaidi ya awali. Na sasa ana ujauzito wa mtoto wetu wa kwanza nina furaha sana.  Haijalishi kwa namna yoyote ile nnavyoonekana ila sasa ni mwanaume mwenye furaha.”
Ila Latif, ambaye hana maumivu na hapati matibabu yoyote, anahofu mtoto wake kama anaweza kuzaliwa na hali kama aliyonayo yeye.
Anasema: “Hatuna uwezo wa kumuona daktari, sisi ni masikini sana. Hakuna daktari kwa siku za nyuma aliyenieleza nisipate mtoto. Ninakuwa na tumaini na kuomba kwamba mtoto wetu atakuwa mwenye afya.”
Kaka yake na Latif aliamua kuuza sehemu ya ardhi miaka minane iliyopita ili aweze kulipia safari ya kwenda kumuona daktari ila hakukuwa na namna ambayo wangeweza kuifanya.
Anakumbuka: “Daktari aliniambia kwamba hali yangu ilitokana na mionzi ya jua wakati mama alipokuwa na ujauzito wangu. Ila sijui kama nahitaji kumuamini.
“Na sasa kuna vitu vingi vinanijia kichwani mwangu kwamba kufanya upasuaji inaweza kuwa ni kitu cha hatari sana.
Nimepoteza tumaini lote la msaada. “Hivi ndivyo nitakavyokuwa daima.”

Shiriki nasi kwa kutoa maoni yako hapa chini

Facebook Blogger Plugin by Michapo Blog

Post a Comment

 
Top