A sign pointing to the Rebecca and John Moores UCSD Cancer Center DNA Sequencing facility at the UCSD in San Diego

Si jambo rahisi kwa mtu yoyote kufanya maamuzi magumu kama haya ambayo wapenzi hawa waliamua kufanya ili tu kutimiza ahadi yao ya kufunga ndoa.
Hayakuwa maamuzi mepesi kwa Jack Beniston kufanya dhidi ya mpenzi wake Michelle wanaoishi Uingereza baada ya kupewa taarifa na madaktari kuwa msichana huyo amebakiza masaa 48 tu kabla hajaaga dunia kutokana na kusumbuliwa na maradhi muda mrefu.
mom
Ndani ya masaa sita baada ya Jack kupewa taarifa hiyo aliamua kuandaa harusi na kuifunga ndani ya chumba cha hospitali ili kutimiza ahadi yake ya kufunga ndoa na binti huyo ambaye alizaa naye mtoto mmoja aitwaye Martha.
Jack aliwaita marafiki pamoja na ndugu zake ambao waliandaa sherehe ndogo ikiwa kumtafutia bibi harusi gauni pamoja na pete ili aweze kutimiza ahadi hiyo.
ringJack alipata sapoti kutoka kwa ndugu zake,marafiki na hata manesi waliokuwa wakimuuguza mpenzi wake ambapo walimwandalia sehemu nzuri akiwa hospitali hapo na hatimaye akafunga ndoa na Jack.
Madaktari walisema Mishelle alikuwa akisumbuliwa na kansa ya kizazi ambayo ilimtesa kwa muda mrefu na mwezi Agust mwaka jana kuhamishiwa katika hospitali ya Peterborough City Hospital ambapo walidai ugonjwa huo tayari umemshambulia kwa kiasi kikubwa na hakuna uwezekano wa kupona
Baada ya kupewa taarifa ya kutoweza kuona na mkewe Jack aliamua kufunga ndoa na Mishelle mwezi September na baada ya kufunga harusi yake alifariki baada ya mwezi mmoja.
groom

Shiriki nasi kwa kutoa maoni yako hapa chini

Facebook Blogger Plugin by Michapo Blog

Post a Comment

 
Top