Shilole na Nuhu Mziwanda
Story ya kwenye U Heard ya leo March 10, inahusu tetesi zilizoenea kuwa wa dada wa mjini akiwemo muigizaji, Jacqueline Wolper wamemchoka msanii Shilole kwa madai kuwa amekuwa akimpiga mpenzi wake Nuh Mziwanda mara kwa mara na wanataka kumtafutia  mpenzi mwingine ambae hatampiga, mpango uliopangwa siku ambayo Shilole alimpiga Nuh na wasanii waliokuwepo kuingilia.
Soudy Brown amemtafuta Shilole na kumpa taarifa hizo na kusema sio kweli ila watu wanazusha ili kuwagombanisha jambo ambalo hawatafanikiwa kwa kuwa anajiamini sana, kwa upande wa  Nuh amesema kuwa ndio kwanza anasikia taarifa hizi ila mwanaume huwa hatafutiwi mwanamke na Shilole hampigi kama wanavyodai zaidi ya kuishi kwa raha.

Shiriki nasi kwa kutoa maoni yako hapa chini

Facebook Blogger Plugin by Michapo Blog

Post a Comment

 
Top